Saturday 14 October 2017

Kuku wa kukaanga na viungo vikavu

Maandalizi; dakika 15
Muda wa kupika; dakika 15
Muda jumla; dakika 30

Mahitaji

Kuku 1 mkubwa
Vijiko 6 vya chakula unga wa ngano
Kijiko 1 cha chakula curry powder
Vijiko 1½ vya chai tangawizi ya unga
Vijiko 2 vya chakula chicken bouillon powder
½ kijiko cha chai pilipili manga
Chumvi kwa kuonja
Mafuta ya kukaangia

Maelekezo

Osha, katakata na kuchanja kuku kisha umpake chumvi
Kwenye sahani pana, weka unga wa ngano, curry powder, chicken bouillon powder, tangawizi ya unga na pilipili manga, changanya vizuri
Paka vipande vya kuku mchanganyiko wa viungo, ishike vizuri kabisa
Kwenye kikaangio katika moto wa wastani (ongeza na kupunguza moto ikibidi) chemsha mafuta. Yakichemka, weka kuku kwenye mafuta, hakikisha hujazi sana kikaangio, acha waive kwa nafasi. Endapo kikaangio ni kidogo, pika kidogokidogo
Kaanga kuku kila upande mpaka awe na rangi ya kahawia au aive vizuri kabisa
Hamishia kwenye wire rack, chujio la bati au karatasi za jikoni ili mafuta yachuje
Pakua kama utakavyopenda
Enjoy

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...