Tuesday 28 November 2017

JINSI YA KUTENGENEZA UBUYU WA ZANZIBAR

UBUYU WA ZANZIBAR
MAHITAJI
1. Sukari vikombe 2
2. Maji vikombe 2
3. Nusu kikombe unga wa ubuyu
4. Vikombe 4 ubuyu wenyewe
5. 1/4 pili pili ya unga
6. 1/4 tsp chumvi
7. 1/4 tsp iliki ya unga
8. Rangi nyekundu au yeyote ile utakavyopenda.
9.vanilla(kama utapenda)

MATAYARISHO
1. Katika sufuria,weka maji na sukari na chumvi na pili pili ya unga na Rangi na iliki. Moto uwe juu kiasi na changanya vyote hivyo vipike vizuri.
2. Wakati vitu vinaanza kujipika utakuta rojo linatoa mapovu. Endelea tu kukoroga acha rojo lipikike vizuri. Baada ya hapo mapovu yakianza kutulia inamaanisha kua rojo limeanza kua zito.
3. Sasa hapo chota kidogo katika mwiko na test kwa vidole kama rojo linanata ua halinati. Rojo linatakiwa linate ndio linakua limeiva. Lisinate Sana kiasi tu.
4. baada ya mchanganyiko wako kuiva ipua hayo maji  sasa Chukua beseni  au sufuria chini  weka ubuyu wako  ndani ya beseni  Anza kumimina hiyo juice yako kidogo kidogo  huku ukiuchanganya kwa mikono safi.Ila hakikisha pembeni una Unga wa ubuyu ulio changanywa na mchanganyiko huo huo.
5.Baada ya ubuyu wako kuchanganyika vizuri (usiwe rojo) Anza kumiminia ule unga kwa juu ili uwe mkavu mkavu na kutoa  ule ubichi  alafu uanike ukishapoa ubuyu tayari kuliwa.
Angalizo: Hatua ya 4 ni muhimu sana hakikisha mchanganyiko unamimina kwenye ubuyu mkavu na sio kuchukua ubuyu mkavu na kuupikia.Tunafanya hivyo ilikufanya ubuyu uwe mlaini na usiwe mgumu wakati wakula.

 MAHITAJI

 1. Sukari vikombe 2 2. Maji vikombe 2 3. Nusu kikombe unga wa ubuyu 4. Vikombe 4 ubuyu wenyewe 5. 1/4 pili pili ya unga 6. 1/4 tsp chumvi 7. 1/4 tsp iliki ya unga 8. Rangi nyekundu au yeyote ile utakavyopenda. 9.vanilla(kama utapenda) MATAYARISHO 1. Katika sufuria,weka maji na sukari na chumvi na pili pili ya unga na Rangi na iliki. Moto uwe juu kiasi na changanya vyote hivyo vipike vizuri. 2. Wakati vitu vinaanza kujipika utakuta rojo linatoa mapovu. Endelea tu kukoroga acha rojo lipikike vizuri. Baada ya hapo mapovu yakianza kutulia inamaanisha kua rojo limeanza kua zito. 3. Sasa hapo chota kidogo katika mwiko na test kwa vidole kama rojo linanata ua halinati. Rojo linatakiwa linate ndio linakua limeiva. Lisinate Sana kiasi tu. 4. baada ya mchanganyiko wako kuiva ipua hayo maji sasa Chukua beseni au sufuria chini weka ubuyu wako ndani ya beseni Anza kumimina hiyo juice yako kidogo kidogo huku ukiuchanganya kwa mikono safi.Ila hakikisha pembeni una Unga wa ubuyu ulio changanywa na mchanganyiko huo huo. 5.Baada ya ubuyu wako kuchanganyika vizuri (usiwe rojo) Anza kumiminia ule unga kwa juu ili uwe mkavu mkavu na kutoa ule ubichi alafu uanike ukishapoa ubuyu tayari kuliwa. Angalizo: Hatua ya 4 ni muhimu sana hakikisha mchanganyiko unamimina kwenye ubuyu mkavu na sio kuchukua ubuyu mkavu na kuupikia.Tunafanya hivyo ilikufanya ubuyu uwe mlaini na usiwe mgumu wakati wakula.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...