Thursday 7 June 2018

Wali wa nazi na maziwa


Wali wa nazi na maziwa

Katika kuvunja miiko ya kuandaa chakula, tuko radhi kutafuta njia tofauti za kupika na kuongeza ladha kwenye mapishi yetu. Haya ni mapishi murua ya kuongeza appetite kwa mlaji.

Mahitaji

  • Mchele 1/2 kilo
  • Nasi ½ kifuu
  • Maji 1 lita (kawaida maji ni mara mbili ya mchele)
  • Chumvi ½ kijiko kidogo cha chai
  • Sour cream (au maziwa ya kawaida ¼ lita)

Maelekezo

  • Andaa tui la nazi kwa kutumia maji ya moto.
  • Osha mchele, ila usiloweke.
  • Bandika mchele jikoni na ongeza chumvi. Acha mchele hadi uanze kuchemka.
  • Baada ya kuanza kuchemka, ongeza tui la nazi pamoja na maziwa. Usikoroge. Acha mchanganyiko uive taratibu kwa takribani dakika 10.
  • Kabla maji hayajaanza kukauka, ongeza maziwa
Maalum kwa wale wanaotumia rice cooker :
Kama unatumia rice cooker ni rahisi zaidi kupika sababu unafanya kila kitu mara moja na unasubiri hadi chakula kiive. Kwenye hatua ya 3. Changanya kila kitu kwa pamoja – mchele, maji yenye tui la nazi, sour cream au maziwa na chumvi. Acha wali hadi uchemke na kuiva.
  •  Pindua chakula ili kiive vizuri. Kama unatumia jiko la mkaa na unapenda kupalilia chakula, ndio wakati umefika sasa.
  • Acha chakula hadi kiive kwa dakika 10 au 15.
N:B Kuna aina tofauti za mapishi ya wali, katika hili wengine wanapenda kuweka tui la nazi wakati wali umeshaiva na wengine wanapenda kuweka wakati wanaanza kupika. Chaguo ni lako. Cha msingi ni kuwa, maziwa yanatakiwa kuingia kwenye wali mapema ili kuweza kuiva na mchele. Hii inaongeza ladha na kuleta harufu nzuri ya chakula maradufu

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...