Friday 6 July 2018

SALTED COOKIES / VILEJA VYA CHUMVI


MAHITAJI 
Siagi vijiko 6 vya chakula
Chumvi kiasi
Viini vya mayai 2
Baking powder kijiko 1 cha chai
Custard powder kijiko 1 cha chakula
Maziwa ya maji vijiko 4 vya chakula 
Unga wa ngano kikombe 1  
Yai 1 la kupakia juu 
Arki unayopenda(nimetumia vanilla na ya chungwa) kijiko ki1 ki1 cha chai 
Ufuta (si lazima)   
Sukari kijiko 1 cha chakula (si lazima)
MATAYARISHO 
  1. Kwenye bakuli weka siagi,maziwa,viini ya mayai , baking powder, custard powder, chumvi,arki na sukari
2.Saga kwa kutumia mwiko,mchapo au machine ya kusagia kwa muda wa dakika 3 hadi 5
  1. Anza kuweka unga wa ngano huku unachanganya 
  1. Unga ukichanganyika ukawa donge , likande kwa dakika 2 hadi 3
  1. Lifunike,liweke  sehem lijivute kwa dakika 7 hadi 10 
 6.pakaza mafuta trey yako 
  1. Baada ya dakika 7 hadi 10 , lisukume kwa kutumia kifimbo cha chapati  mpaka uwe size , isiwe nyembamba sana 
 8. Kata kwa kutumia kifaa chochote cha kukatia vileja 
  1. Vipange kwenye trey , vipakaze yai juu na ufuta 
10 . Vichome kwa oven moto 180°c kwa dakika 10 hadi 15 au mpaka uone vimewiva na kubadilika rangi,  vitoe (manjano ilokoza)
*Unaweza kutumia mkaa pia kuokea. 
ENJOY NA CHAI AU KAHAWA  

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...