Wednesday 4 July 2018

SAMAKI WA MCHUZI


SAMAKI WA MCHUZI

MAHITAJI


 Samaki vipande 3 ( unaweza kutumia samaki yoyote vizuri akiwa hana miba)

 Kitunguu thomu 1 tsp ( garlic paste) Tangawizi 1 tsp (gigger paste) Pilipili manga 1 tbs (black papper) Chumvi kiasi Ndimu kiasi Bizari manjano 1/2 tsp Bizari nzima ya unga 1/2 tsp Tungule 2 kubwa ( nyanya chopped) Bilingani 1/2 size ( chopped) Masala ya pilau 1/2 tsp Mafuta 4 tbsp Pilipili ya kuwasha 1 Maji ya kiasi 

MATAYARISHO

 kwenye sufuria yako ya kupikia mchuzi weka samaki wako uliowaosha vizuri roweka na spice zote kwa muda wa nusu saa au hata zaidi sio mbaya.baada ya nusu saa weka tungule zako (nyanya) bilingani na mafuta kwenye samaki wako ulomroweka acha vichemke pamoja kwa dakika 10. 

Sasa weka maji kiasi yafunike samaki wako tu acha vichemke mpaka maji yapungue na samaki wako aive onja chumvi na ndimu kama unahitaji zaidi unatengeza, weka pilipili yako ya kuwasha acha ichemke na mchuzi kwa dakika 2 mpaka 3 na mchuzi wako utakuwa tayari.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...