Thursday 30 August 2018

Pai Ya Viazi Na Nyama Ya Kusaga

Pai Ya Viazi Na Nyama Ya Kusaga

Vipimo
Nyama ya kusaga                                      1½ lb (ratili)
Kitunguu                                                   1 Kikubwa
Thomu na tangawizi                                   1 Kijiko cha supu
Mboga upendayo
(karoti, mahindi, na kadhalika)                    1- 2 Kikombe
Viazi                                                          1½ – 2 lb (ratili)
Siagi                                                          ½ Kikombe
Kidonge cha supu kilichoyeyushwa               ½ Kikombe maji
Worcestershire sauce au yoyote nyingine      1 Kijiko
Chumvi                                                      kiasi
Mchanganyiko wa bizari                              1 Kijiko cha supu
Jibini (cheese) ya iliyochunwa (grated)        1 gilasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1.       Menya maganda ya viazi na katakata, kisha chemsha katika maji yenye chumvi hadi viwive.
2.       Wakati viazi vinaiiva, yeyusha nusu ya ile kipimo cha siagi katika sufuria kisha kaanga kitunguu hadi ilainike.
3.       Kisha tia thomu na tangawizi.
4.       Halafu tia nyama ya kusaga na ukaange hadi isiwe nyekundu tena.
5.       Weka mboga, chumvi na bizari zilizobakia na iachie moto mdogo kwa muda iive vizuri.
6.       Ponda viazi pamoja na ile siagi iliyobakia, kisha ongeza chumvi na pilipili manga ikiwa haijakolea.
7.       Tandaza kwanza viazi kisha mchanganyiko wa nyama katika treya ya oveni kisha tandaza tena viazi vilivyopondwa kwa kutumia uma ili iwe na dizaini upendayo.
8.  Mwagia jibini (cheese) juu yake.
9..       Pika katika oveni yenye moto wa 400° kwa muda wa dakika 30 hivi na ubadilisha moto wa juu katika dakika 5 za mwisho ili igeuke rangi ya kupendeza juu.
10..       Epua na tayari kuliwa.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...