Maandalizi; dakika 15
Muda wa kupika; dakika 15
Muda jumla; dakika 30
Muda wa kupika; dakika 15
Muda jumla; dakika 30
Mahitaji
Kwa viazi vya kukaanga

Nusu kilo viazi
Vijiko 3 vya chakula corn flour/ corn starch
Chumvi kwa kuonja
Mafuta ya kukaangia
Vijiko 3 vya chakula corn flour/ corn starch
Chumvi kwa kuonja
Mafuta ya kukaangia
Kwa ajili ya sauce

Kijiko 1 cha chai tangawizi na kitunguu saumu
Vijiko 2 vya chakula asali
Kijiko 1 cha chakula mafuta ya kupikia
Kijiko 1 cha chakula sosi ya soya
Vijiko 2 vya chakula chili sauce
½ pilipili hoho nyekundu
Kijiko 1 cha chai hoisin sauce (ukipenda)
¼ kikombe majani ya kitunguu
Vijiko 2 vya chakula asali
Kijiko 1 cha chakula mafuta ya kupikia
Kijiko 1 cha chakula sosi ya soya
Vijiko 2 vya chakula chili sauce
½ pilipili hoho nyekundu
Kijiko 1 cha chai hoisin sauce (ukipenda)
¼ kikombe majani ya kitunguu
Maelekezo

Kwenye bakuli kubwa, weka viazi na chumvi. Changanya vizuri, kisha ongeza corn flour, changanya vizuri

Chemsha mafuta kwenye kikaangio moto wa juu kiasi. Ongeza viazi, kaanga mpaka viive na viwe vya rangi ya kahawia. Kumbuka kugeuza mara unapoweka kwenye mafuta visishikane. Toa kwenye mafuta, chuja mafuta

Kwenye kikaango kingine, weka mafuta kijiko 1 cha chakula. Yakichemka ongeza kitunguu saumu na tangawizi. Kaanga kwa sekunde kama 30 kisha weka pilipili hoho uikaange kwa dakika kama 2 halafu weka majani ya kitunguu

Ongeza asali, hoisin sauce, sosi ya soya na chilli sauce. Kanga kwa dakika 1 nyingine

Ongeza viazi vilivyokaangwa. Changanya vizuri sosi ikolee kwenye viazi

Pakua cha moto

No comments:
Post a Comment