Thursday 18 January 2018

Jinsi ya kupika Rosti ya maini ya ngo´mbe

Matayarisho; dakika 15
Muda wa kupika; dakika 20
Muda jumla; dakika 35

Mahitaji

500g/ nusu kilo ya maini
Vijiko 4 vya chakula mafuta ya kupikia
Kijiko 1 cha chai tangawizi
Kijiko 1 cha chai kitunguu saumu
Hoho mchanganyiko nusu x3
Karoti 1
Nyanya 2 za wastani
Kitunguu maji 1 cha wastani
Pilipili kichaa 1
Chumvi kwa kuonja
Majani ya giligilani (ukipenda)

Maelekezo

Weka nyanya na pilipili kwenye mashine ya chakula utengeneze rojo
Menya, osha na katakata maini; katakata kitunguu maji, pilipili hoho na karoti vipande vidogovidogo vya mraba; twanga kitunguu saumu na tangawizi; katakata majani ya giligilani
Kwenye sufuria au kikaango kikubwa katika moto mkali kiasi, weka mafuta. Ongeza kitunguu maji, kitunguu saumu na tangawizi. Kaanga kwa dakika kama 2, au mpaka viive vizuri ila visikauke
Ongeza maini. Weka na chumvi kwa kukadiria. Endelea kukaanga huku ukigeuza geuza hadi maini yapate rangi ya kahawia kiasi, ila yasiive kabisa
Ongeza rojo ya nyanya na pilipili. Funika acha iive kwa moto wa wastani mpaka nyanya ziive vizuri, dakika kama 4
Ongeza karoti kwa dakika kama 1 kisha weka pilipili hoho kwa dakika nyingine 1; au mpaka viive kama utakavyopenda. Unaweza pia kuongeza maji kidogo ukipenda mchuzi
Pakua kama utakavyopenda
Enjoy

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...