SAMAKI WA MCHUZI
MAHITAJI
Samaki vipande 3 ( unaweza kutumia samaki yoyote vizuri akiwa hana miba)
Kitunguu thomu 1 tsp ( garlic paste) Tangawizi 1 tsp (gigger paste) Pilipili manga 1 tbs (black papper) Chumvi kiasi Ndimu kiasi Bizari manjano 1/2 tsp Bizari nzima ya unga 1/2 tsp Tungule 2 kubwa ( nyanya chopped) Bilingani 1/2 size ( chopped) Masala ya pilau 1/2 tsp Mafuta 4 tbsp Pilipili ya kuwasha 1 Maji ya kiasi
MATAYARISHO
kwenye sufuria yako ya kupikia mchuzi weka samaki wako uliowaosha vizuri roweka na spice zote kwa muda wa nusu saa au hata zaidi sio mbaya.baada ya nusu saa weka tungule zako (nyanya) bilingani na mafuta kwenye samaki wako ulomroweka acha vichemke pamoja kwa dakika 10.
Sasa weka maji kiasi yafunike samaki wako tu acha vichemke mpaka maji yapungue na samaki wako aive onja chumvi na ndimu kama unahitaji zaidi unatengeza, weka pilipili yako ya kuwasha acha ichemke na mchuzi kwa dakika 2 mpaka 3 na mchuzi wako utakuwa tayari.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO
JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...
-
JINSI YA KUPIKA CHAPATI LAINI MAANDALIZI/PREPARATION 1.Kwanza hakikisha unakanda unga vizuri Make sure you knead the dough very well...
-
Urojo ni mchanganyiko wa vyakula mbali mbali pamoja na uji uji wake katika bakuli moja. Hapa nitaeleza jinsi ya kuupika huo uji(urojo) m...
-
MAHITAJI/INGREDIENTS 1.Nyama ya kusaga kilo kasorobo(3/4) 3/4 Kg Minced Meat 2.Kitunguu maji kikubwa 1 1 Medium size Onion 3.Ker...

No comments:
Post a Comment