Friday 20 October 2017

UNAJUA KUPIKA PILAU YA KUKU??

PILAU YA KUKU 

MAHITAJI

 Mchele magi 1 1/2 Vitunguu maji 3 medium (vikate) Chembe 7 za karafuu Bizari nzima (cumin) 1 tbsp Vijiti 4 vya mdalasini viwe vya size 1 tbsp chumvi 1 tsp chopped tangawizi 1 tsp chopped garlic Mbatata 3 za medium( kata vipande 6) 1 tsp masala ya pilau 1 tsp hiliki powder B paper nzima 1 tsp Baby chiken 1 mkate 6 piece Mafuta 1/4 kikombe cha chai

 MATAYARISHO

Loweka mchele wako kwa muda wa saa 1 au mawili.osha kuku wako vizuri mchemshe kwenye dish mtie garlic, tangawizi chumvi, karafuu na vijiti vya mdalasini weka maji ya kutosha kuku aive na supu ibakie kama mug 3 kwaajili ya kupikia wali. 

Weka mafuta yako kwenye dish nyingine ya kupikia pilau yako tia vitunguu ulokata kaanga mpaka vikianza kupiga rangi kidogo weka uzile mzima, black paper nzima, hiliki powder, masala ya pilau na mbatata. Kaanga pamoja mpaka vitunguu vyako ukiviona viko tayari.sasa weka supu yako bila kuku acha ichemke mpaka mbatata zikianza kuiva nusu tu lakini hapo weka kuku wako onja chumvi kama unahitaji zaidi utaongeza. Weka mchele wako acha uchemke huku unakoroga mpaka supu yote ikauke na mchele wako utakuwa umeiva nusu. Sasa weka kwenye oven funika kwa foil au mfuniko, moto 160 mpaka pilau yako ikauke na iive vizuri sasa toa pakua na enjoy na salad na pilipili.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...