Sunday 24 June 2018

JINSI YA KUPIKA VISHETI,AMA KUANDAA VISHETI


.VISHETI 

MAHITAJ

I siagi 100gm Sukari 100gm Maziwa ya unga 2 tbls Baking powder 1ts Unga wa ngano 400gm Yai 1 Vanilla 2 ts Mafuta ya kupikia nusu litre Casta sugar (sukari ilosagwa) nusu mug. Kwa ajili ya shira

 MATAYARISHO

 Saga sukari na siagi pamoja mpaka ilainike weka yai.mix vizuri halafu weka unga, vanila kijiko kimoja, baking powder na unga wa maziwa changanya vizuri.weka maji kidogo kidogo kwenye mchanganyiko wako mpaka uwe donge moja tizama usirowe na wala usiwe mgumu sana. Ugawe sehemu 8 chukua kila sehemu sokota kama kamba na ukate vipande vidogo vidogo.weka mafuta kwenye jiko yakipata moto weka visheti vyako (deep fry) mpaka viive visiwe vyekundu sana.toa viweke pembeni vipoe. Weka dish kwenye jiko weka maji nusu mug na casta sugar.acha ichemke mpaka iwe nzito ( utaona inaaza kuganda pembeni mwa dish) weka vanilla na visheti punguza moto speed ya mwisho. Mix mpaka viwe vikavu kabisa (vizuri kuvi mix kwa kuliinuwa dish na kuvipeta ili visivurugike). Tayari kwa kuliwa kwa kahawa au kuwapa wageni wakija.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...