Sunday 10 June 2018

MAPISHI: Keki Ya Walnut (Jozi) Na Mdalasini

   
Vipimo:
Unga  mweupe                                             1 ½ kikombe
Siagi                                                            10 vijiko vya supu
Sukari ya brown (soft brown sugar)              ½ kikombe
Baking powder                                             1 ¾  kijiko cha chai
Mayai                                                           2
Maziwa                                                        ¼ kikombe
Walnut zilokatwakatwa (chopped)                1 kikombe
Mdalasini wa unga                                        1 kijiko cha chai
Chumvi                                                        ¼ kijiko cha chai
Vanilla                                                        ½ kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
  1. Weka siagi nje iwe laini (katika room temperature)
  1. Washa jiko la oveni kiasi cha 350°
  1. Weka siagi katika bakuli ipige hadi iwe laini.
  1. Tia mayai uendelee kupiga
  1. Tia vitu vikavu vyote .
  1. Tia maziwa kisha walnuts  
  1. Paka siagi katika treya ya kupikia keki iwe size ya kiasi inchi 8 au 9
  1. Mimina mchanganyiko wa keki
Pika kwa muda wa dakika 35-40,  iangalie kama imeiva kwa kutia kijiti na kukitoa ikiwa kavu tayari, epua na iache ipoe.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...