Sunday 30 September 2018

Pizza yenye topping ya kuku na cheese



Pizza, chakula rahisi kuandaa unachoweza kula wakati wowote - asubuhi, mchana au usiku. Ni vizuri kuandaa siku unayotaka kula chakula na kupumzika vizuri ukiwa unaongea na familia, marafiki au wengine Ni chakula chepesi, chenye virutubisho vingi na pia ni kitamu sana. Unaweza kuongeza vitu unavyopenda kuipendezesha pizza yako. Mapishi haya yameandaliwa na nnjosie, asante kwa kutushirikisha kwenye kujiramba na utamu wa misosi.

Kuandaa: dakika 75
Mapishi: dakika 35

Mahitaji
Kwa ajili ya unga:

Vijiko 2 vya chai vya hamira (yeast)
Vikombe 1 ¾ vya unga wa ngano. Tenganisha, weka kidogo pembeni
¾ ya kikombe cha maji ya uvuguvugu
Chumvi kijiko 1 cha chai
½ kijiko cha mafuta ya Olive (Mafuta ya mizeituni)
Kwa ajili ya topping:

Minofu ya kuku
Mixed  herbs vijiko 2 vya chakula
Nyanya 2 kubwa
Pilipili hoho 1 na nusu
Mozzarella cheese
Kitunguu saumu vijiko 3 vya chakula vilivyosagwa
Butter vijiko 2 vya chakula
Pilipili manga kijiko 1 cha chai

Mapishi haya ya pizza unayoweza kuandaa kirahisi nyumbani yameandaliwa na nnjosie. Kwa ujumla pizza hii imeandaliwa kwa kufuata maelezo kama ilivyoandikwa hapa, lakini imetumia topping ya kuku, butter, mozarella na pilipili manga.

Andaa pizza kama ilivyoezwa hapa.
Pasha oven nyuzi joto 350°F (180°C). Bandika minofu ya kuku jikoni, acha ichemke kwa dakika 15. Weka pembeni ipoe.
Kwenye kikango, weka butter acha iyeyuke, kisha weka kitunguu saumu kijiko 1, mixed herbs na pilipili manga. Epua acha ipoe weka kwenye friji kwa muda.
Sambaza butter iliyotoka kwenye friji juu ya pizza kwa tumia kijiko. Weka kuku, nyanya, pilipili hoho kisha nyunyizia kitunguu saumu. Weka mozzarella cheese na nyunyizia mixed herbs. Oka Pizza kwa dakika 15 mpaka 20.
Epua. Jirambe.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...