Saturday 6 October 2018

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO


TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI
TAMU SANA KWA LADHA KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA


MAHITAJI

2 paketi za spaghetti 
60 gram olive oil 
1kitunguu maji kikubwa, chop chop
5 gram kitunguu swaumu
240 gram nyanya ndogo ndogo kata nusu
1 kijko cha chai unga wa coriander
1 kijiko kidogo cha chai unga wa cumin
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa turmeric 
240 gram za chickpeas (Kumbuka kuhifadhi maji utakayochemshia) 
1 kijiko kikubwa cha chakula tomato paste 
6 au 7 mbegu za green olives(sio lazima) 
1 fungu la majani ya giligilani na majani ya mint kwajili ya kupambia
60 gram  korosho au karanga
5 gram chumvi

    JINSI YA KUPIKA FATILIA PICHA NA MAELEKEZO HAPO CHINI



    Chemsha chickpeas ziive kabisa ziwe laini kisha chuja maji na . Zichemshe spaghetti fuata maelekezo katika paketi yake. Kisha kaanga vitunguu katika mafuta pamoja na kitunguu swaumu mpaka vilainike.



    Ongezea zile nyanya ndogo ndogo ulizokata nusu, tomato paste pamoja na viungo vyote kaanga mpaka upate harufu nzuri ya mchanganyiko wako kuiva na kua rojo rojo .



    Kisha ongezea chickpeas na kaanga kwa dakika 2 au 3



    KIsha weka spaghetti zilizochemshwa, olive oil, olives na korosho kisha endelea kukoroga pole pole.


    Kisha juu yake pamba kwa kutumia majani ya gili gilani na mint. Majani haya yanaongeza harufu safi na ladha nzuri sana, korosho au karanga zinakupa crunch safi sana.




    FURAHIA MLO HUU RAHISI MTAMU NA SAFI SANA KWA AFYA YA MLAJI

    JINSI YA KUANDAA NA KUPIKA TAMBI ZA DENGU NYUMBANI.

     
    Mahitaji : 🔸Unga wa dengu kilo 1

    🔸Chumvi kiasi
    🔸Pilipili manga kiasi
    🔸Pilipili ya unga kiasi
    🔸Manjano kijiko 1 cha chai
    🔸Baking soda 1/2 kijiko cha chai
    🔸Mafuta ya kula  kikombe 1
    🔸Maji vugu vugu kiasi cha kukandia

    NAMNA YA KUTAYARISHA:

    1. Changanya vitu vikavu vyote vizuri katika bakuli, tia mafuta kisha changanya tena ufanye chenga.

    2. Anza kutia maji taratibu hadi upate unga mlaini, paka mikono yako mafuta kisha kanda unga kwa muda wa dk 5

    3. Funika na uache ukae kwa muda muda wa dk 10. Bandika mafuta jikoni juu ya moto wa kiasi

    4. Utie unga wako katika mashine ya tambi kisha binya taratibu kuruhusu tambi kutoka na kudondoka kama mvua katika mafuta ya moto kisha taratibu zungusha mzunguko mmoja na acha ziive na kupata rangi pande zote mbili (angalia picha katika comments)

    5. Epua katika chujio zichuje mafuta, rudia utaratibu kwa unga wote. Taratibu zivunje vunje na tambi zako zitakuwa tayari kwa kula.

    MTAG RAFIKI YAKO AJE AJIFUNZE PISHI JIPYA.

    Tuesday 2 October 2018

    JIFUNZE KUPIKA VITUMBUA KITAALAMU.


    VITUMBUA

     MAHITAJI 

    Mchele kikombe (mug) 1 Hamira 1 and 1/ 2 tsp Hiliki 1/2 tsp Sukari 1/2 kikombe Tui la nazi zito 3/4 kikombe about 200 ml Unga wa ngano 2 tblsp Yai 1 Mafuta ya kupikia 

    MATAYARISHO 

    Loweka mchele usiku mzima angalau masaa 5 au zaidi.weka mchele, hamira, tui la nazi na hiliki kwenye blender saga kwa dakika 5 weka unga wa ngano halafu saga tena mpaka mchele uwe laini.

     Pumzisha blender kila baada ya dakika 3. (unatumia kama dakika 10 mpaka uwe laini). 

    Mimina kwenye bakuli weka maji vijiko 2 vikubwa kwenye sukari ikoroge mpaka ichanganyike halafu mimina kwenye batter (mchanganyiko wa mchele).mix vizuri mpaka uhisi sukari imeyayuka.acha batter yako iumuke. Ikisha kuumuka piga yai vizuri (kama hupendi harufu ya yai basi changanya yai na kijiko kimoja cha maziwa hivi inakata harufu). 

    Yai likisha kupigika vizuri changanya kwenye batter yako mix vizuri,tayari kwa kuchomwa. Weka chuma kwenye jiko tia mafuta kwenye chuma weka batter yako choma vitumbua kwa moto wa kati ukiona vinaungua punguza moto.

    WAZAZI: Chakula kizuri kwa mtoto/ CHAKULA BORA KWA MTOTO MDOGO/ CHAKULA MAALUMU KWA WATOTO WA DODO/ MAMA NA MTOTO.

    Kutokana na kuwa na utumbo mdogo, watoto hawali sana.Ndio maana ni muhimu kuwa na uhakika wa chakula wanachokula kina lishe nyingi za kutosha na zote.Jifunze au jua jinsi ya kuweka muda wa kula kwa watoto ili wapate hizo lishe bora kwao.

    Muda wa mzuri wa kula
    Kiujumla,chakula cha nguvu ni kwa kuanzia watoto wa miezi sita (6)na kuendelea,pindi kinapoandaliwa zingatia akili ya ulaji wa mtoto wako.Lakini vizuri pia uzungumze na mkunga au daktari wa watoto kabla ya kumpa mayai,samaki,citrus,na maziwa ya mtindi kama mtoto wako mdogo chini ya mwaka kwasababu vyakula hivyo huweza kusababisha allergy.Vyakula vingine kama nyama,matunda,na mboga mboga huweza kuanza kumlisha mtoto wa miezi 6 .Ila kumbuka vyakula hivyo vya aina yoyote kisitambulishwe kwa mtoto wa miezi mine(4).

    Japokuwa watoto hukua kwa utofauti,ni vizuri kutafuta ushauri wa daktari au watu wazima dawa wale, kwa kujihakikishia pindi unapotaka kumuanzishia chakula mtoto na pia kipi ni bora zaidi kwa huyo mtoto wako.

    Ndizi
    Ndizi zina wanga (carbohydrates) mwingi,amabayo hutia nguvu,vile vile fiber kwa kusuport kulainisha mmeng’enyo chakula tumboni.Ni kizuri na chepesi kuwa chakula cha mtoto,na huwa rahisi kuiva kwake.Pindi unapoandaa ndizi kwa mtoto mdogo,hakikisha imeiva vizuri na imepondeka vizuri.Kwa mtoto mkubwa anaweza kula ndizi kama ilivo yaani nzima,lakini iwe pia imeiva vizuri iwe rahisi kwa mtoto kuisaga na kuimeza kwa urahisi zaidi.
    banana.jpg

    Viazi vitamu
    Viazi vitamu ni kizuri chenye chanzo ya potassium, vitamin C, na fiber na wingi wa beta-carotene, ni antioxidant ambayo husaidia kulinda aina za magonjwa cancer na kusafisha free radicals.Watoto wengi hupenda viazi vitamu zaidi kuliko mboga mboga kwasababu ya ladha yake ya utamu wa asili.Pindi unapopika hivi viazi viponde au kusaga,viazi vitamu ina ulaini ambao ni rahisi kwa mtoto kuvila,hata kwa watoto ambao ndo wanaanzishiwa kula solids au vyakula vigumu.
     Sweet-Potatoes-3.jpg
    Thanksgiving-2011_TM1B54-mashed-sweet-potatoes_s4x3.jpg

    Parachichi(avocado)
    avocado-mixed.jpg

    Parachichi wakati mwingine huwa kama mboga,lakini hilo ni tunda!Ina lishe nyingi kuliko aina ya vyakula vingine vifananavyo na parachichi.Parachichi lina protini nyingi katika mafungu ya matunda na ni tajiri wa mafuta (fat)-“ni nzuri” aina hii ya mafuta inavilinda vidudu au diseases vya ugonjwa wa moyo.Hakikisha unampa mtoto parachichi liloiva vizuri .Osha nje ya hilo tunda,kisha menya maganda na lisage liwe laini.Sababu lina mafuta mengi kwahiyo mara moja mtoto kushiba,mpe kidogo na chakula kingine,huweza kuwa kuku au nyama laini.

    Mayai
    IMG_1356.jpg
    Mayai ni mazuri.Yai leupe huwa ni protein tu na kiini kina zinc na vitamins A, D, E, na B12.
    Kiini pia kina choline, research inaonyesha ni nzuri kwa afya ya maendeleo ya kukuza akili.Kimila,madaktari wa watoto huwa wanashauri walezi wasiwape watoto mayai—na sana sana ile nyeupe—mpaka baada ya mwaka kwa sababu ya matokeo ya alergy.

    Lakini huo ushauri kwa sasa umebadilika,na baadhi ya wataalam wanaamini kwamba mayai yacheleweshwe kwa familia ambazo zina historia ya matatizo ya allergy.Wakati mayai ni chanzo kikuu cha protein na lishe nyingi nyingine,shauriana na mtaalam wako pindi mtoto wako ameanza kula vyakula kuangalia kama ni sawa au kipindi gani itafaa kumpa mayai mtoto wako.
    Kwa upande wangu nashauri mayai mazuri ni ya kienyeji na sio ya kuku wa kisasa au kizungu kwa sababu ya dawa na muda wa utotolewaji wake pia ni mdogo.


    karoti

    DSC_0375_2311.jpg
    karoti ina wingi wa beta-carotene, na antioxidant ambayo hutoa ile rangi ya orange.Beta-carotene hubadilishwa kuwa vitamin A mwilini na huchukua nafasi ya kukuza ukuaji na afya ya kuona.Kupika karoti huleta ladha ya asili yake ya utamu,ambayo hupendwa na watoto sana,ambao wamezaliwa wanapenda ladha ya vitu vitamu.Unapoandaa karoti kwa mtoto mdogo,hakikisha zinaiva sana hadi kuwa laini.Kama mtoto mkubwa na anweza kula ikiwa nzima ilioiva haijalainika huwa nzuri zaidi,unaweza kumlisha ilopikwa kidogo tu.


    Maziwa ya mtindi
    making-yogurt-30.jpg
    Maziwa ya mtindi humpatia mtoto calcium, protein, na phosphorus,ambazo ni muhimu kwa kukamavu au kutia nguvu,mifupa yenye afya na meno. Maziwa ya mtindi yana probiotics,ni aina ya bacteria mzuri ambae anasidia katika mfumo wa usagaji chakula na kusupoti immune system. Watoto wanahitaji sana mafuta katika mlo wao,kwahiyo chagua maziwa mazuri ya mtindi ambayo yana mfuta kidogo,au yana aina ya mafuta tofauti tofauti .

    Pia epuka maziwa ya mtindi ya ladha au flavored,ambayo huwa yana sukari nyingi.Kama unahisi kuongezea ladha,changanya na matunda yalosagwa.Mtoto chini ya umri wa mwaka huweza kuwa na matokeo mabaya ya protein inayopatikana kwenye maziwa ya mtindi,usisite kushauriana na daktari wa mtoto wako kabla hujampatia maziwa hayo .


    Baby cereal
    neslac-rice.jpg
    Iron-fortified infant cereals humpa mtoto wako madini ya chuma yanayotakiwa katika ukuaji wake. Watoto huzaliwa na madini ya chuma,lakini huanza kupungua au kuisha kuanzia miezi5-6.Maziwa ya mama hayana hayo madini ya kutosha,ni muhimu kutengeneza vyakula vyenye hayo madini chuma.

    Kama mtoto wako ameanza kula vyakula,wataalam wengi wanashauri iron-fortified rice cereal ni chakula cha mwanzo kwa sababu ni aghalabu kuleta au sababisha allergy kama nafaka nyingine.Pindi mtoto anaendelea kukua,unaweza kuchanganya infant cereal na matunda.Ni vizuri ikawa laini au nyepesi na matunda kama pear, peach,na plum.

    Cheese
    dsc_0352.jpg
    Cheese ni nzuri yenye protein –ni muhimu kwa ukuaji-- na calcium kwa kujenga mifupa imara na meno. Cheese ina dose ya afya ya riboflavin (vitamin B2),ambayo husaidia kubadili protein, fat, na carbohydrates katika mfumo wa nguvu au energy. Swiss cheese kwa kawaida ni tamu na laini kwa watoto.Japo cheese huweza kuwa choking hazard,au kukatwa vipande pande. Ni nzuri kwa watoto wanaokula vitu vizima kama kidole na hutumika kwa vitu vingine pia .


    kuku
    dsc02771.jpg
    kuku ana protein na ni chanzo cha vitamin B6,amabayo hutumika kusaidia kutia nguvu mwilini tokea kwenye vyakula.Ni muhimu kwa watoto kuanza kula mara kwa mara chakula chenye protein hata kwa uchache wake kusaidia ukuaji wa mtoto.Kama mtoto wako hapendi ladha ya kuku ile yenyewe,mchanganyie na matunda anayopenda au mboga anayoipenda.

    Citrus fruits
    img_6323.jpg
    Citrus fruits, ikiwemo chungwa, ndimu, na zabibu,ni nzuri na chanzo cha vitamin C,ambayo husaidia kutengeneza collagen inayopatikana kwenye mishipa ,mifupa,na tissues nyingine mwilini. Vitamin C pia huponesha palipoumia na kusaidia kuyeyuka kwa madini chuma kutokea kwenye vyakula vingine. Citrus fruits pia ina potassium, madini amabyo yanasiadia misuli kujikunja na kufanya kazi vizuri na kumaintain afya ya fluid balance mwilini.kuwa makini acid isizidi kwa mtoto,ni vizuri zaidi kutompa mtoto citrus fruits mpaka baada ya kutimiza au baada ya mwaka.

    citrus-fruits.jpg

    Nyama nyekundu(red meat)
    6a0115721bb963970b0147e2333e09970b-pi.jpg
    Nyama nyekundu huleta kwa urahisi ya kuyeyusha aina ya madini chuma kwa mtoto wako.Madini chuma husaidia seli za damu nyekundu kubeba Oxygen kwenda kwenye seli kupitia mwilini na ni muhimu kwa kukuza akili au ubongo.Kwa bahati mbaya,upungufu wa madini chuma –ambayo huweza sababisha madhara katika usomaji na tabia pia-ni moja wapo ya upungufu wa lishe kawaida kwa watoto.

    Ndio maana ni muhimu kuhakikisha mtoto wako anayapata haya madini chuma,kutokea kwenye nyama nyekundu,na vyanzo vingine katika mlo wake.Kwa watoto wadogo,weka nyama yenyewe haswa,kama beef na karoti.Watoto wakubwa ambao wanaweza kutafuna ipike vizuri kisha watumie hivyo.


    Butternut Squash
    Butternut-Squash-Soup-11.jpg
    Butternut squash ni nzuri kwa watoto sababu wanapenda ladha ya utamu.Ni chanzo kizuri cha antioxidant beta-carotene na pia ina vitamin C, potassium, fiber, folate, B-vitamins,na ina omega-3 fatty acids.Ni rahisi kutayarisha nyumbani kama utanunua ilo prepeeled, precut squash inayopatikana wanapotengeneza.Chemsha ichemke vizuri,kisha ikoroge mpaka ilainike.Tengeneza na uwaandalie kwa familia ni nzuri sana na ina ladha nzuri pia.


    Samaki
    smoked-haddock-2.jpg

    Samaki weupe,kama vile haddock na cod,ni wazuri sana kwa protein,ambayo watoto wanaihitajia kwa maendeleo ya kukua. Samaki wa mafuta , kama salmon, huleta fat-soluble vitamins na mafuta yenyewe fats, kama DHA,ambayo inakuza akili na macho na kukuza mfumo wa immune. Samaki huweza sababisha allergy,kwahiyo ongea na mtaalam wa watoto kabla hujampatia mwanao.Kama iko POA,basi utamsababishia mtoto afya nzuri.Wataalam wanashauri ni vizuri kumlisha mtoto samaki mara mbili katika mlo wake kwa wiki yenye mercury kidogo,kwakuwa ina faida nyingi za kiafya kwa mtoto.

    Nyanya
    Image result for nyanya
    Nyanya ina lycopene nyingi, pigment nyekundu katika nyanya ina fanya kazi kama antioxidant kusaidia kulinda na cansa na vijidudu vya moyo. Lycopene huweza kuyeyeuka ikafanya kazi vizuri mwilini kama nyanya itakua imepikwa vizuri na mafuta.Kwahiyo tengeneza sauce ya tomato na tambi kwa kupika nyanya na mafuta ya olive oil.Saga iwe laini kwa watoto wanaoanza kula.Sauce ya kutengeneza nyumbani ina sukari,na chumvi kidogo kuliko ya kununua,na ni nzuri kwa familia yote.Hivi huna tomato fresh?basi hata za kwenye makopo ni nzuri pia.

    Peas/Njegere
    Image result for njegere
    Peas huwa ina burst pamoja na vitamin K,lishe ambazo zinafanya kazi pamoja nazo ni calcium husaidia kujenga mifupa. Peas ni chanzo cha antioxidant vitamins A na C, na pia folic acid B vitamins. Na kumuwekea peas mtoto kwenye sahani yake ita boost fiber katika mlo wake,na ni muhimu sababu wataalam wameona watoto wote na hata na watoto wakubwa pia,hawapati fiber ya kutosha.Kusaga chakula cha watoto basi peas ni rahisi sana .



    Broccoli
    Broccoli-Garlic-Hazelnuts.jpg
    Broccoli ni kwakweli ni chakula kizuri ,ni chanzo kikuu cha vitamin C na pia ina beta-carotene, folic acid, madini chuma, potassium, na fiber.Kuchemsha broccoli katika maji hupunguza karibu nusu yake ya vitamin C ilokuwemo, kwahiyo ni vizuri kuisteam au kuweka kwenye microwave. Kama mwanao nimpenzi wa ladha ya broccoli,mchanganyie na kitu kitamu au mboga anayoipenda ,kama viazi vitamu au butternut squash.


    Tambi(pasta)-makaroni

    shutterstock_81645955.jpg
    Tambi ina carbohydrates nyingi,ambayo huvunjwa vunjwa kusambaza guvu mwilini.Na ina ladha nzuri na ziko za shape nyingi tofauti tofauti zenye fun kibao,ambazo huvutia kwa watoto wa rika zote.Tambi nyingi zina vitamins na madini, kama folic acid,madini chuma, and B-vitamins. Ni mchanganyiko wa nafaka na ngano nzima ina fiber, lakini texture yake huweza kuwa nzito kwa mtoto .Tambi zenye shepu au umbo dogo dogo zipikwe vizuri hadi zilainike huwa ni chakula kizuri kwa watoto hata wakubwa kubwa pia mdogo.




    WAZAZI: Chakula kizuri kwa mtoto/CHAKULA BORA KWA MTOTO MDOGO/ CHAKULA MAALUMU KWA WATOTO WA DODO/ MAMA NA MTOTO.

    JINSI YA KUTENGEZA JUICE YA MCHANGANYIKO WA TIKITI NA LIMAO.


    MAHITAJI
    450 grams Vipande vya Watermelon vyenye ubaridi,
    250 gram ya maji ya dafu au Nazi changa
    1 limao kubwa
    10 vipande vya barafu au Ice cubes,
    Fresh Mint kwajili ya kupambia

    Kata nusu tikiti maji zuri lililoiva kama unavyoona kwenye picha kisha likate kate vipande na uweke kwenye friji vipoe kabla ya kutengeneza juisi yako

    Chukua maji ya dafu, limao, vipande vya barafu na vipande vya tikiti maji kisha weka kwenye blender. Lengo la kuweka limao ni kuongeza na kubalance ladha. kama wewe ni mpenzi sana wa maji ya madafu unaweza ongeza zaidi ili ladha ya madafu isikike sana.
    Blend vizuri mpaka vitu vyote vichanganyike safi kabisa.

    Perfect drink for your summer, waandalie familia wafurahie pia kama unabiashara waandalie wateja wako wafurahie sana hasa kipindi hiki cha majira ya joto. kumbuka tikiti maji na dafu vyote vinasukari kwahiyo huna haja ya kuongeza sukari kabisa na ukafurahia kinywaji hiki murua.
    tarimkyeAsante

    JINSI YA KUANDAA NA KUPIKA KATLESI ZA SAMAKI.



    Vipimo

    Viazi - 5 kiasi

    Tuna - 2 vikopo

    Carrot - 1

    Pilipili mboga - Nusu

    Kitunguu saumu(thomu/galic) - ½ kijiko cha chai

    Pilipili - kiasi

    Chumvi - kiasi

    Ndimu - kiasi

    Unga wa ngano - ½ kikombe

    Yai - 1

    Mafuta ya kupikia - Kiasi

    Namna ya kutayarisha na kupika

    Menya Viazi uvichemshe na chumvi.

    Vikiwiva vichuje maji, viponde ponde, vilainikie – weka kando

    Chuna carrot ziwe kama chicha, kata pilipili mboga  nyembamba nyembamba, fungua vibati vya Tuna kamua majia yake mwaga.Changanya Tuna, carrot, pilipili mb

    oga, thomu, pilipili kali, chumvi, ndimu, kisha uchanganye na viazi ulivyoviponda. Hakikisha vimechanganyika vizuri.

    Tengeneza vidonge kiasi unachotaka na kata umbo unalopenda kama la yai au duwara ukimaliza weka pembeni.

    Changanya unga na maji uwe mzito mzito tena uchanganye vizuri na yai.

    Weka karai katika moto, mimina mafuta kama ya maandazi, kisha chukua vidonge chovya katika unga uliochanganywa yai  na utumbukize ndani ya mafuta yaliopashika moto vizuri.

    Ziwache mpaka zibadilike rangu, uzitoe. Tayari kwa kula.

    #mapishi #mapishigram #mapishiyetu
    v_massalaAsante ,Ya yai me nataka jmn
    middmach75@mrs_middmach
    ackrina_kadiliAsante, mara ya mwisho nilipika katlesi za nyama ya kusaga, lkn nilitengeneza shimo katika nikaeka nyama ya kusaga, wakati wa kukaanga mafuta yalikua haya fiki katikati
    annyjaycob3sawa sawa @mapishigram lakn io tuna ndo nn ?? naomba nieleweshe mmakonde mimi
    ackrina_kadiliNitajaribu kwa namna hii, bt tuna kwangu itakua ngumu so I'll try nyama ya kusaga kwa namna hii. Asante kipenzi I appreciate ua good work
    dadamzalendoNaomba na recipe ya cutless za viazi mpendwa
    asha.ramahsamaki mbona sijaona unachanganya mdacgan
    abiolaskids_jlovely

    JINSI YA KUANDAA NA KUPIKA SAMBUSA ZA NYAMA.



    Vipimo

    Manda ya sambusa ya tayari - Kiasi zinavyouzwa(Kiasi ya sambusa 40-50)

    Mafuta ya kukaangia - Kiasi

    Nyama ya Kusaga - 3LB (Pounds)

    Kitunguu saumu(thomu) na tangawizi iliyosagwa - 2 Vijiko vha chai

    Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chai

    Pilipili manga - 1 kijiko cha supu

    Garam masala - 1 kijiko cha supu

    Chumvi - Kiasi

    Vitunguu maji vilivyokatwa (chopped) - 3 Vidogo au 2  Vikubwa

    Kotmiri iliyokatwa (chopped) - Kiasi

    Namna ya kutayarisha na kupika

    Pika nyama ya kusagwa kwa kutia chumvi, thomu na tangawizi, pilipili na ndimu.

    Kabla haija kauka tia Garam masala.

    Zima moto acha kidogo ipoe tia vitunguu na kotimiri.

    Funga sambusa katika manda kama kawaida.

    Pika sambusa katika mafuta ya moto hadi ziwe nyekundu na zikiwa tayari kuliwa.

    #mapishi #mapishigram #mapishiyetu
    hamisa_ally95Asante kwa kutu fundisha naomba kuulza swal mbona mm niki pika sambusa zikiwa , za moto znakua ngumu kama kaukau zikipoa zina tepeta ngamba la nje nakosea wap

    JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

    JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...