Monday 2 July 2018

Jinsi ya kupika wali wa manjano

[​IMG]

Mahitaji
  • 1 au 2 Saffron ( zafarani ya orange)
  • 4 kijiko kikubwa cha chakula Olive oil
  • 1 kitunguu kikubwa kata kata
  • 1 pili pli hoho katak kata vipande vidogo vidogo
  • 1 kijiko kidogo cha chai kitunguu swaumu cha kupondwa
  • 240 gram mchele wa basmati
  • 340 ml za maji ya vugu vugu
  • 5 gram ya chumvi
  • Majani kiasi ya giligilani kwa ajili kupambia na kuongeza ladha

Jinsi ya kupika
  1. Washa jiko lako katika moto mdogo, weka kikaango chako kwenye moto kisha weka mafuta, kitunguu maji na safron pamoja na endelea kukaanga pole pole.
  2. Baada ya mafuta kubadilika rangi ya machungwa yatoe katika moto na acha ipoe kwa dakika 10 kisha yachuje hayo mafuta.
  3. Chukua kijiko kimoja kikubwa cha mafuta na weka katika kikaango. Kisha chukua tena kitunguu maji na kitunguu swaumu endelea kukaanga mpaka vilainike. Kisha ongeza pili pli hoho na endelea kukaanga mpaka iwe laini.
  4. Kisha weka mchele na endelea kukaanga pole pole mpaka mchele utaponukia na kubadilika rangi na kulainika.
  5. Ongeza maji na ufunike iendelee kuiva kwa dakika 8-10 kwa moto mdogo mpaka iive.
  6. Baada ya kuiva kataka majani ya corriender na pamba katika wali wako.
  7. Unaweza kuongeza ladha ya chakula hiki kwa kuweka karanga au zabibu kavu au hata korosho kavu.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...