Monday 2 July 2018

Jinsi ya kupika wali wa njegere




[​IMG]

Mahitaji

  • 240 gram mchele wa Basmati
  • 120 gram njegele za kumenywa (chickpeas)
  • 3 majani ya kitunguu maji (spring onions), kata kata
  • 1 fungu la giligilani chop chop
  • 1 fungu la parsley chop chop
  • 1 kijiko kikubwa cha cakula siagi (butter) kwakuongeza ladha ya chakula
  • Chumvi kulingana na ladha upendayo

Jinsi ya kupika
  1. Chukua kikaango weka siagi ikisha ikiyeyuka weka majani kiasi ya kitunguu maji na uendelee kukaanga. Kisha chuja mchelewako wa basmati nao weka ukiwa mkavu na endelea kukaanga mpaka unukie.
  2. Weka chumvi pamoja na njegere koroga kiasi.
  3. Kisha weka maji safi 400 ml (hii inategemea na kiwango cha mchele wako) kisha funika mfuniko wa kikaango au sufuria yako na pika kwa dakika 10.
  4. Weka chop parsley na chop giligilani kisha koroga zichanganyike na wali wako.
  5. Baada ya hapo wali wako utakua umeiva na unaweza kula na mboga yoyote upendayo.

No comments:

Post a Comment

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...