Tuesday 3 July 2018

Jinsi ya kupika wali wa soseji na mboga za majani


[​IMG]

Mahitaji

  • 3 vipande vya sausage
  • 1 fungu la majani ya vitunguu
  • 1 kitunguu kikubwa
  • 100 gram njegere
  • 500 gram chele basmati
  • 5 gram chumvi
  • 5 gram pili pili manga

Jinsi ya kupika

  1. Weka mafuta ya kupikia kwenye kikaango chako kisha weka vitunguu maji na uvikaange.
  2. Ongezea majani mabichi ya vitunguu na uendelee kukaanga hadi vitoe harufu na sio kuungua au kubadilika rangi.
  3. Weka mchele na ukaange kwa dakika 3 mpaka 4 kisha weka maji ya wastani yazidi mchele wako kiasi na uendelee kukoroga ili maji yachanganyike na mchele wako.
  4. Funikia na weka moto wa wastani ili wali wako uive taratibu.
  5. chukua sausage zako na kata kata vipande vidogo kisha weka juu ya wali wako njegere zilizochemshwa pamoja na vipande vyoote vya soseji.
  6. Kumbuka kuendelea kukoroga ili kila kitu kichanganyike, pia kama wewe ni mpenzi wa blue band au samli unaweza weka kiasi ili kuongeza ladha na harufu katika wali wako.
  7. Baada ya dakika 45 wali wako utakua umeiva kama haujaiva basi ongezea maji kidogo na endelea kupika katika moto mdogo.

1 comment:

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI TAMU SANA KWA...